Sawa lyrics

  2024-06-28 01:15:16

Sawa lyrics

It's Bonga

(Oh nah nah nah nah nah aah)

Asante Mungu Baba uliye mwema

Nimeiona siku nyingine ya furaha

Hali sio haba sio njema

Wa kuniponya nipate hata chembe ya furaha

Maana wazazi wananitegemea

Na ninakaribia mi kuitwa Baba

Nami ndunguzo waloegemea

Sina kitu nimechalala nimevava

Uniepushe mabaya dunia

Yasijenikumba

Napiga goti kwa uchungu nalia

Ni nusuru muumba

Katu nisikate tamaa

Niende kusaka tonge

Nipate ama nishinde njaa

Moyoni upige konde, ni sawa eh!

Ni sawa, ni sawa

Nami nitafika (Ata nikikosa sawa)

Ni sawa, ni sawa

Nami mimi utanipa (Ah ridhiki we ndo unayegawa)

Sawa, ni sawa

Nami nitafika (Mwanadamu hawezi panga)

Ni sawa, ni sawa

Nami mimi utanipa (Sitozuguka kwa waganga)

Natapa tapa elimu sina

Mi kusoma sijasoma

Nami nasaka nijenge heshima

Mi nakoma ju wananichoma

Ni wewe pekee ndo naye jua

Ah mbele yangu na nyuma yangu

Mie mpweke naomba dua

Ah Baba fungua ridhiki zangu

Nashukuru Baba, pumzi unayonipa

Maisha naendelea

Ila kingine Baba, nadhalilika

Huu mzigo unanielemea

Baba niwewe Baba (Ni wewe)

Niwe ndo msaada (Ni wewe)

Ni wewe, ni wewe

Baba ni wewe

Uniepushe mabaya dunia

Yasijenikumba

Napiga goti kwa uchungu nalia

Ni nusuru muumba

Katu sikate tamaa

Niende kusaka tonge

Nipate ama nishinde njaa

Moyoni upige konde

Ni sawa, ni sawa

Nami nitafika (Ata nikikosa sawa)

Ni sawa, ni sawa

Nami mimi utanipa (Ah ridhiki we ndo unayegawa)

Sawa, ni sawa

Nami nitafika (Mwanadamu hawezi panga)

Ni sawa, ni sawa

Nami mimi utanipa (Sitozuguka kwa waganga)

See more
Ibraah more
  • country:Tanzania
  • Languages:Swahili, English
  • Genre:
  • Official site:
  • Wiki:
Ibraah Lyrics more
Excellent recommendation
Popular
Copyright 2023-2024 - www.lyricf.com All Rights Reserved